1. Jijini Dar
chorus
Misele ya Kinondoni, ya Temeke, ya Ilala
Jijini Dar-es-Salaam
Nikakatizia Tanga, Mwanza, Kigoma, Tabora nikarudi
Jijini Dar-es-Salaam
Kona za Buguruni, Kariakoo, mpaka Posta
Jijini Dar-es-Salaam
Nikakatizia Zenji, Mombasa, Kampala, Kapirimposhi nikarudi
Jijini Dar-es-Salaam
Misele ya Mwananyamala, ya Manzese na Ubungo
Jijini Dar-es-Salaam
Nimefika mpaka China, Urusi, Ujerumani, Marekani nikarudi
Jijini Dar-es-Salaam
Mimi ni msafiri bado niko njiani, ninakokwenda nitafika maana ninakujua
Verse 1
Tangu sabini na nane, usiku wa manane
Darda King nilishuka ulimwenguni nimenyane
Muumba aliniambia dunia ina mwenyewe
Ukipita salama, thawabu yako itakuwa nawe
Barabara kuu ya hali ngumu na mvua ya mawe
Ni heri vyenye mabawa virukavyo kama mwewe
Utajiri utamchagua nani kati ya mimi na wewe aah!
Mzichi! asiye na mwana aeleke jiwe
Mfalme ni Mfalme himayani kwangu nitawale
Nina mabingwa wa sanaa maonyesho na vitendo tele
Usilete za kuleta na hadithi za Kalumakenge
Wanahanya wapate menyu Mazichi wana unenge
Miaka ya themanini wacha hisia zitupagae
Wasanii walipotajwa kama Sikinde ngoma ya ukae
Kwenye tisini feni likapepea mbele
Miondoko ya kikongo ilipodundwa na Kabasele
Karne ya ishirini na moja nakuja kama mpira wa kona
Wanakuja kichwa kichwa babu sijapata kuona
Duniani Darda King mimi ni bado msafiri
Popote nitokeako mazichi mnipokee
Repeat chorus
Verse 2
Masafa ya ndani na nje, ki Vasco da Gama
Farasi alipogoma mi kwa ngondi nilichoma
Some times nikala boda kwa boda kama Osama
Dunia nzima nakumbushia Hiroshima
Mabibi na mabwana amini tu ninachosema
Nimekutana na watu mashuhuri tena noma
Nelson Mandela mzee wa heshima
Dunia nzima imempatia vema
Mu'Ammar Gadafi mzee wa mitikasi,
Fidel Castro kila dakika yuko wima
Wasanii wa muziki wakali waliovuma
Mos Def, Hide wa Japan, Remmy wa Matimila
Wana masumbwi wagumu kama chuma
Tyson, Isangura nao wakina Matumula
Wanakabumbu vinara waliojituma
Makumbi Juma, Malota Soma, Gaga na Kihwelu Musa
Mwanakikapu hatari niliyemwita MJ
Akitisha akiruka kimetinga
Duniani Darda King mimi ni bado Msafiri
Popote nitokeako Mazichi mnipokee
Repeat chorus
2.Kanazi
Chorus
Hivyo ndivyo vituko vya mtaa wa Kanazi
Watoto wanacheza
Hivyo ndivyo vituko vya mtaa wa Kanazi
Wengine wanalia
Hivyo ndivyo vituko vya mtaa wa Kanazi
Oya! bingwa umeiona hiyoo
Hivyo ndivyo vituko vya mtaa wa Kanazi
Verse 1
Nyumba namba saba mtaa wa kanazi
Ndipo walipokuwa wanaminya wakimbizi
Miaka sita saba wakatuachia sisi
Banda la uwani nikawa napigia ndizi, Mzichi
Sasa nimeshaota mizizi
Mtaani ni kama nahodha wa jahazi
Wacha nimzukie Suzi
Hapa geto ninaona mambo gozigozi
Naingia mtaani, watoto kwa wazee wananipigia pozi
Vijana wana bling rangi zao za mavazi
Mademu wame chill wanajisikia luuziii
Bado nawavutia pumzi
Najua siku moja nitapata mapenzi
Dukani nikapate mbili dozi
Kisha nizunguke nikamwone Babu chizi
Kugeuka wanamkimbiza mwizi
Mshike mshike wakampiga kitanzi
Wakati Pafi kazunguka kusaka kazi
Pati twenty four anadunda tumbo wazi
Wakatu Shubi yuko chuo kwenye kozi
Bado mama Chuki ana supply maandazi
Ya leo babu kubwa, cha mtoto ya juzi
Huo ndio msemo wa mtaa wa Kanazi
Repeat chorus
Verse 2
Kanisa la Kibatisti kwa nyuma kuna uwazi
Ndipo Liver Pool wanapopigia tizi
Japo kuna visiki na magoli ya miti
Mazichi kila jioni wana lisukuma gozi
Siku ya mechi kali wote wana jezi
Refa ni mvinje bwana hataki ushenzi
Leta za kuleta utateguliwa tezi
Jebu kali mpaka ubongo utakufa ganzi
Edi Baba anakaanga viazi
Mama ntilie anachachua mchuzi
Seremala anakusanya vibanzi
Watoto wa mama Roda bado wanadaka panzi
Anti Juli shoga yake na Nazizi
Yuko kichochoroni analichunua buzi
Baba anambatua mama Nyamizi
Amemfumania na Chale muuza nazi
Jamila macho yanamtoka machozi
Ameshapewa mimba na mjumbe wa nyumba kumi
Bora nikajichanganye vijana jazz
Kusiko na mabraza-meni ambao hawa chezi
Ya leo babu kubwa, cha mtoto ya juzi
Huo ndio msemo wa mtaa wa Kanazi
Ya leo babu kubwa, cha mtoto ya juzi
Huo ndio msemo wa mtaa wa kanazi
3 Tulingeba
Intro
Astaghafiru-llah, Nimerudi Darda King
Mfalme mwenye hekima na maarifa
Napenda kuchukua nafasi hii
Kuitambulisha miondoko ya Tulingeba
Ulimwenguni kote, kutoka Dar-es-Salaam
Wakina mama kedekede naona wanayo hamu
Wanakatika wakisikilizia utamu
Morani matumbo wazi long time
Wanaruka juu na kutua kwa zamu zamu
Chezeni pamoja wote binadamu
Kata mauno mpaka chini chamgamsha damu
Oya! Mzichi mbona hauchezi?
Ah! Darda King nataka cheza bila Demu!
Ninakuja nayo midundo ya tulingeba
Imeshashika chati kama banchikicha
Huko Beijing wananiambia shieh shieh
Jamaica wananipa ya-man!
Amerika wamebaki midomo wazi
Afrika nasikia wananchi hawalali
Mazichi wangu mabibi na mabwana
Viuno legeza tucheze tulingeba
(Tulingeba yoyo)x3 tulingeba
Tunakuomba wewe dada uje hapa
Tukuone maringo yako, maringo yako
{(bingiri)x5 mpaka chini} x8
(Tulingeba yoyo) x3 tulingeba
Tunakuomba wewe kaka uje hapa
Tukuone maringo yako, maringo yako
{(bingiri)x5 mpaka chini} x8
Ah! wacha bwana, Darda King
Midundo live, Houston Texas represent Bongo
4. Zaburi 23
Intro
Naam, nijapopita katika bonde la uvuli wa mauti
Sitaogopa mabaya maana Wewe upo pamoja nami
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji
Verse I
Sidhani kama nina tena mpinzani
Maana peke yangu Mfalme nimebaki
Na hata kama kuna wanaotaka upinzani
Mpaka nikiondoka vijakazi watabaki
Na kila mimi nilalapo kitandani
Maono ninaona ya wanao nidhihaki
Na kila mimi nisimamapo jukwaani
Furaha naleta kwa wapendao burudani
Naona wapo wanaotaka ushindani
Mimi ni Mfalme wafuasi watabaki
Ee Bwana, kama wametoka Ushenzini
Waeleze Dardanus ni Mfalme aliyebaki
Na kila Darda King nikaapo enzini
Milango nafungua kwa wanaotenda haki
Na kila Darda King niwapo mikasini
Ni mishindo ya kushindua kama mkuki
Amini chochote kinitokacho kinywani
Maana siwezi kukwambia nisichojua
Jua linapokuwa kali napiga miwani
Kofia ya bazuka inaponyesha mvua
Moshi wa mjani uko hewani
Hatua mbili mbele tatu nyuma mchoroni
Na mijicho myekundu mitaani
Vichochoro nikunje nitokee Kinondoni
Afande akizuum ninunue pikipiki
Vikinishinda nivitupie machakani
Nikimtoka nipige misele miwili
Niruke ukuta niibukie maskani
(Nilishaumwa na nyoka, nikiona unyasi ninashituka
Nilishakubwa na dhoruba, na bado baharini mimi nitavuka)x2
(Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha ya Darda King)x6
Verse 2
Nasikia wapo wanaonong'onanong'ona
Wanaosema mimi ni Mfalme gani
Nasikia wapo wanaotokotatokota
Chora michoro kuniweka kizuizini
Nipeleke kwa pilato ukidhani nina kosa
Nitalipa akinishika na hatia
Amenawa na amesema sina makosa
Amesuuza mikono, sina hatia
Ushahidi wa makosa mkikosa
Ya bandia mwaanza nibandikia
Wapambe nuksi nasema sina makosa
Ya nini mabango mnanishikia
Joho langu linang'ara kwa weupe
Mbona madoa mnataka kulitia
Kitabu changu kina kurasa nyeupe
Mbona madhambi mnakiandikia
Mimi ni Mfalme mwenye hekima
Nilikuwepo nipo na bado nitakuwepo
Mimi ni kama yule Msamaria mwema
Nilikubeba walipopita kama upepo
Mazichi wote duniani wamenikubali
Tangu nilipokuja na nani kama mama
Huko kwa Kibaki mimi ni kama almasi
Tangu nilipodunda midundo ya Nairobi
Mwanaume maneno naweka kando
Na kama nikisema ujue kuna vitendo
Nimeamua niwe kama kondoo
Nimeshamaliza lakini mambo bado
(Nilishaumwa na nyoka, nikiona unyasi ninashituka
Nilishakubwa na dhoruba, na bado baharini mimi nitavuka)x2
5. Kaburu
Ye ye ye yea, Darda King, Kaburu
Ndani ya nyumba, hakuna shaka kata shingo
Mfua chuma pata shika, seke seke
Mwaga majalo kama Yanga na Simba
Mpira kati tupa kitu, huyu Kaburu
kuwa makini kama hivi
Utangulizi umenielewa mimi ni nani
Sina utani Kaburu napora pipi kwa mtoto
Chezee moto wa tipa nakupa kubwa
Kuwa mbishi utapigwa ndizi
Maji ya shingo toka mbio
Hii ni fani nyingine bwana mbali na kazi
Kula bia, pata mjani, kula chaki na shika mic
Mwaga radhi, hizi raba nyingine
Kama hivi kama vile, mimi na Darda
Nagonga hodi, (bom)x3 ndani ya Bronco mpaka bongo
Kata nyodo, watoto oo ooh Kaburu amekita mjini
Hapakaliki mbindembinde mshikemshike
Wanoko mpishe nakupa misheni
Pata fuba zungusha kamata nyumba 745
Funga mguu 23 kama babu wape tabu
Waliokuona wewe ni kavu, wanalia chumvi
Wanakula vumbi kushoto kulia tupige bia
Hamna vita, dili limeitika msela kashinda
Machoko mjini mmekwisha
6. YiHo!!!
(YiHo!!! YiHo!!!)x2
Verse1
Kama una ki-blauzi kipige mkunjo
Piga machejo onyesha manjonjo
Kama ni khanga moja nipigie fundo
Kwenye ki-sketi kata mauno
Shega shega tingisha mabega
Shika kamata kama ni ya moto mwaga
Saga saga rumba mpaka majogoo
Msaada kwenye tuta, sooo
Mazichi wanayumbayumba na kujigusagusa
Pa jipangusangusa kwa jikwaruzaruza
Wanaburudikadika kwa kujirusharusha
Kisha wanasema hiyo ni safi safi
Kila mtu na demu wake fakdat
Babu yangu kamata wawili
Naona mambo yamenoga waa waaat
Ona wanavyonipigia makofi
Mademu wanashushashusha na kubinukanuka
Sha jishanuanua, re jirembuambua
Wanajisikiakia kwa kujishikashika
Kisha wanasema Darda King
Wanataka niwapakate
Tugandane kama siagi na mkate
Wanataka niwape mate
Mazichi wananipigia makofi
Chorus
(Ninaimba verse Imbeni kiitikio YiHo!!! YiHo!!!)x2
YiHo!!! vimwana tingisheni makalio YiHo!!! YiHo!!!
YiHo!!! mazichi zungusheni visigino YiHo!!! YiHo!!!
Verse 2
Kama una manoti nyanyua mikono
Zungumza kwa pesa na sio mdomo
Mapigo babu kubwa pasipo mfano
Kuanzia Alhamisi mpaka Jumatano
Vunja mifupa wakati una meno
Yakibaki mapengo fungua mabano
Ukiwa arosto tuliza mshono
Potelea mbali wakitutolea mfano
Kama una mkoko weka mikono juu sema YiHo!!!
Kama unalo geto weka mikono juu sema YiHo!!!
Kama hauna demu weka mikono juu sema YiHo!!!
Kama hauna meni weka mikono juu sema YiHo!!!
Kama unapuliza weka moto juu
kimbiza mwenge uweke kuleleni juu
Kama ni wa mitungi tuone chupa juu
Kisimu cha mkononi nacho kiweke juu
Ukipagawa njoo hapa juu
Kapelo yako iweke juu
Ukinogewa njoo hapa juu
Na hilo shati lako nalo liweke juu
Repeat chorus
